Jumamosi, 3 Septemba 2016
Na:Fadhila Kizigo>>> Mashindano Ya Netball Taifa Yafana

Kuelekea Fainali ya Netball kitaifa Mkoani Morogoro matokeo ya mechi ambazo zimechezwa
Jeshi-Star Vs TTPL 54-59, CMTU Vs Uhamiaji 22-71, Madini Vs Kinondoni 85-5, Polisi Arusha Vs Jiji Tanga 59=30, Arusha City Vs Ras-Kagera 85-35. Jeshi Star Vs Kinondoni 102-14, CMTU Vs Jiji Tanga 65-33, Polisi Moro Vs Madini 69-14 Polisi Arusha Vs Arusha City 54-43.
Kauli Ya Makonda Baada ya Kuahirisha UKUTA
Ni August 31, 2016 ambapo Chama cha Demokrasia Na Maendeleo Chadema kilitangaza kuahirisha mikutano, maandamano ya UKUTA kwa mwezi mmoja ili kutoa fursa kwa viongozi wa dini kutafuta muafaka. Aidha mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amezungumza baada ya chama hicho kuahirisha maandamano ya ukuta 'Maandamano hayajawahi kujenga shule, maandamano hayajawahi kuleta elimu, maandamano hayajawahi kushusha vitu bei maduka bali Maandamano ni Vurugu yaani kuondoka Amani na wale wanaodai demokrasia wanapaswa kwenda kutii tu kanuni zao za Bunge' Kwaiyo kwenye mkoa wetu si tu tarehe 1 basi hakuna mtu kuzurura mahali popote pale, Ukuta ni kiwango cha mwisho cha mtu kufikiri sasa ndio maana wenzetu wameshindwa mwisho wa siku wanatafuta fursa kwa viongozi wa dini kutafuta muafaka' 'Mimi nafikiri naomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania afanye kazi na atekeleze aliyoyasema kipindi cha uchaguzi ili vijana tufanye kazi katika viwanda mbalimbali tuachane na mambo ya UKUTA bali tuangalie vitu vya maendeleo'
Ijumaa, 2 Septemba 2016
Headline Za Magazeti Leo Sept 3
Jumatano, 31 Agosti 2016
Na:Fadhila Kizigo>>Polisi Arusha Waanza Vyema Netball
Timu ya Polisi Arusha ya Netball yaanza vyema michuano ya Netball dhidi ya Tumbaku Morogoro . polisi Arusha imeanza vyema michuano hiyo kwa kuifunga Tumbaku kwa seti 59 kwa 56. Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti kamati ya ufundi kitaifa Asha Sapi amesema kuwa licha ya timu 10 kutoshiriki kati ya 21 nikutokana na uhaba wa kifedha. Aidha Sapi amesema kuwa timu zimeanza vyema kwa kuwa na nidhamu kwa waamuzi.
Na:Fadhila Kizigo>>>Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro Laimarishwa
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro limeimarisha viungo kwa kufanya mazoezi maeneo ya manispaa ya Morogoro. Akizungumza na waandishin wa habari kamanda wa Polisi Mkoani Morogoro Ulrich Matei amesema kuwa mazoezi hayo yamelengwa kwa kuimarisha jeshi na si vinginevyo. Pia kamanda Matei amesema kuwa siku ya kesho wananchi wasiwe na hofu kwani jeshi letu limeimarishwa vyema kwa ulinzi hivyo maandamano hayo ni ya kichochezi hivyo ameomba wananchi kutokuwa na hofu kwani jeshi la polisi limeshakamata wale ambao ni wachochezi na wanaendelea kukamata kwa watakaoleta uchochezi wa maandamano.
Jumanne, 30 Agosti 2016
Na:Fadhila Kizigo>> Mh Kebwe Azindua Mashindano Ya Netball Morogoro
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Steven Kebwe amezindua Rasmi mashindano ya Netball ligi dalaja la kwanza katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro. Mashindano hayo yatakayofanyika viwanja vya Jamhuri mkoani humo yamezinduliwa kwa Mikoa mbalimbali kushiriki michuano hiyo. Hata hivyo Mh.Kebwe ametoa wito kwa taasisi mbalimbali kuunga mkono suala la michezo kwani lipo kisheria na kufanya hivyo ni kujenga taifa la wanamichezo lakini pia Kebwe ameomba vijana kupambana na Ukimwi ili kujenga nguvu kazi ya Taifa.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)




