Kampuni ya Chemi and cotex industries limited invites washeherekea miaka 25 ya kutumia dawa ya meno aina ya whitedent kampeni hiyo imezinduliwa, na Mkuu wa Wilaya ya Musoma mjini Dr.Vicent Anney. Aidha kampuni hiyo imewashukuru watanzania kwa kutumia dawa ya meno ya whitedent na kwa kuwarudishia shukrani wao kama kampuni wameamua kutoa shindano la gari ambalo magari zaidi 300 yanashindaniwa katika mikoa yote Tanzania. Kwa upande wake Meneja wa kampuni hiyo kwa tawi la mkoa wa Mara Mr. Govind Singh alisema "Kampuni imejipanga kufanya mambo mazuri kwa watumiaji wa bidhaa zao". hata hivyo meneja aliongezea kwa kusema kuwa kila kitu kitaenda vizuri katika kuendesha shindano hilo la kugombania gari aina ya toyota saloon. Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Musoma Mjini Dr.Vicent Anney alisema "pamoja na kualikwa katika hafla fupi hiyo amekuwa na tatizo la madawati katika wilaya yake na kuchukua nafasi hiyo kuwaomba kampuni ya Chemi and Cotex kuchangia madawati katika wilaya hiyo kwani kwa kufanya hivyo kutawaamasisha watu kutumia bidhaa zao". Mashindano hayo yanaendelea Nchi nzima kwa watanzania wote kuchukua fomu na kujaza kisha unabashiri viboksi ambavyo vipo kwenye gari kwa kubashiri mara nyingi zaidi baada ya hapo unaweza ukachaguliwa kuingia kwenye droo na ukajishindia gari.
Jumamosi, 9 Julai 2016
Whitedent Washeherekea miaka 25 Kwa Kugawa Magari?
Kampuni ya Chemi and cotex industries limited invites washeherekea miaka 25 ya kutumia dawa ya meno aina ya whitedent kampeni hiyo imezinduliwa, na Mkuu wa Wilaya ya Musoma mjini Dr.Vicent Anney. Aidha kampuni hiyo imewashukuru watanzania kwa kutumia dawa ya meno ya whitedent na kwa kuwarudishia shukrani wao kama kampuni wameamua kutoa shindano la gari ambalo magari zaidi 300 yanashindaniwa katika mikoa yote Tanzania. Kwa upande wake Meneja wa kampuni hiyo kwa tawi la mkoa wa Mara Mr. Govind Singh alisema "Kampuni imejipanga kufanya mambo mazuri kwa watumiaji wa bidhaa zao". hata hivyo meneja aliongezea kwa kusema kuwa kila kitu kitaenda vizuri katika kuendesha shindano hilo la kugombania gari aina ya toyota saloon. Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Musoma Mjini Dr.Vicent Anney alisema "pamoja na kualikwa katika hafla fupi hiyo amekuwa na tatizo la madawati katika wilaya yake na kuchukua nafasi hiyo kuwaomba kampuni ya Chemi and Cotex kuchangia madawati katika wilaya hiyo kwani kwa kufanya hivyo kutawaamasisha watu kutumia bidhaa zao". Mashindano hayo yanaendelea Nchi nzima kwa watanzania wote kuchukua fomu na kujaza kisha unabashiri viboksi ambavyo vipo kwenye gari kwa kubashiri mara nyingi zaidi baada ya hapo unaweza ukachaguliwa kuingia kwenye droo na ukajishindia gari.
Jumatatu, 4 Julai 2016
Jike Shupa wa Kwenye Tv awa Kiki Mjini
Msanii wa filamu nchini Zena Haji alimaarufu Jike shupa ameingia kwenye headline kwa haraka sana mara baada ya kushirikishwa katika video ya wimbo wa msanii wa bongo Freva Nuhu Mziwanda uitwao Jike shupa. Msanii huyo ambaye alishiriki kama video queen katika wimbo huo ambao unafanya vizuri sana katika media mbalimbali nchini Alisema "Napata matatizo sana kutokana na wimbo huo kwa baadhi ya watu kunifananisha na Shilole". Zena Haji aliongezea kwa kusema kuwa tangu wimbo wa jike shupa umeachiwa hewani amekuwa akipata meseji nyingi sana kutoka kwa mashabiki wake wakimpongeza kwa kufanya vizuri katika wimbo huo pia amekuwa akipata interview nyingi sana katika media mbalimbali kutokana na wimbo huo wa jike shupa. Mwisho alimalizia kwa kusema kuwa wantanzania wasimchukulie kweli kama ana tabia hiyo ila mwisho wa siku ibaki kuwa ni kazi kama kazi nyingine na heshima ibaki kuwa pale pale pia mrembo huyo aliwataka mashabiki wake wakae tayari kwa vitu vizuri kutoka kwake kwani ana matarajio makubwa sana kwa ivi karibuni cha msingi ni mkumuomba mwenyezi Mungu hatufikishe alisema msanii huyo.
DEAL DONE KWA CHELSEA
Klabu ya Chelsea ambayo msimu ujao itaanza kunolewa na aliyekuwa kocha wa wa timu ya taifa ya Italia katika michuano ya Euro 2016 Antonio Conte, imetangaza rasmi kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Ubelgiji aliyekuwa anaichezea Marseille Michy Batshuayi. Michy Batshuayi mwenye umri wa miaka 22 ametangazwa na Chelsea na kusaini mkataba wa miaka mitano ya kuishi ndani ya stamford bridge London England.
Alhamisi, 30 Juni 2016
Kubenea na Joseph Mbilinyi Wasimamishwa kuhudhuria bungeni.

Mbunge wa Ubungo Chadema amesimamishwa kuhudhuria vikao vitano vya bunge na Naibu spika Dk Tulia Akson baada ya kubainika kusema uongo kwamba Waziri wa Ulinzi na JKT Dk Hussein Mwinyi ameingia Mkataba na kampuni ya China Henan International Cooperation Group Company wa ujenzi wa nyumba za JWTZ na nyumba ya Waziri huyo jambo ambalo sio kweli. Pia Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi amesimamishwa kuhudhuria vikao kumi vya bunge kuanzia leo june 30 mwaka huu baada ya kubainika kunyosha kidole cha kati kwa wabunge baada ya kukiri mbele ya kamati ya Haki, Maadili na Madaraka kwamba alifanya kitendo hicho. Hata baada ya kuhojiwa Mbunge Mbilinyi alishindwa kumtaja Mbunge wa CCM aliyedaiwa kumtukana ili naye achukuliwe hatua na kamati hiyo. Bunge limeridhia adhabu hiyo iliyotolewa na kamati.
Maguli apata Dili Uarabuni.

Alhamisi, 16 Juni 2016
Fainali Ya Mashindano Ya Kuhifadhi Qur'an tukuf Yaanza Rasmi Jumapili
Assalam aleykum, Aisha Sururu Foundation inayo furaha kuwaalika kwenye fainali ya mashindano ya mwaka 2016 (1437 AH) ya kuhifadhi Qur'an tukufu itakayofanyika jumapili ya tarehe 19/06/2016 katika ukumbi wa Diamond jubilee Hall jijini Dar es salaam, ambapo vijana wanawake na wanaume watakaoshiriki katika mashindano haya watapigania nafasi zao za kwanza kwenye jukwaa la mashindano ya kuhifadhi Qur'an katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan. Mashindano ya kuhifadhi Qur'an ya mwaka huu yatakuwa ni mashindano ya kumi na nne (14) tangu mashindano ya kuhifadhi Qur'an yanayoandaliwa na Aisha Sururu Foundation yaanzishe, Alhamdulillah. Mwaka huu Aisha Sururu Foundation imeshirikisha mikoa 24 ya Tanzania pamoja na visiwa vya Zanzibar, Unguja na Pemba, kwa nia ya kuwashajiisha watoto kuhifadhi Qur'an katika viwango vya juu vya kuisoma Qur'an tukufu. Kauli mbiu ya mwaka huu: Tuwathamini Walimu Wetu wa Qur'an Tukufu, Tupate Radhi za Mola Wetu Ra'ufu.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)



